Tuesday 26 January 2016

SEHEMU YA PILI

Hatua ya pili

Katika hatua hii tulianza rasmi kulinda mimea yetu dhidi ya wadudu na magonjwa mbalimbali,na mbaka muda huo tulikua tunajua adui zetu wakubwa ni ukungu pamoja na utitiri(mwekundu au mweusi),hivyo tulinunua madawa ya ukungu pamoja na madawa ya kuua wadudu wanaoweza kushambulia mimea yetu.Tulikuwa tukipulizia dawa ya ukungu mara moja kwa wiki na hata dawa ya wadudu(sumu)tulipulizia mara moja kwa wiki.Lakini hizi dawa hazikutumika kwa wakati mmoja,sumu ya wadudu ilitumika peke yake kwa wakati wake(siku tofauti)na dawa ya ukungu ilitumika tofauti kwa wakati wake.Wakati huo huo kazi ya umwagiliaji iliendelea kama kawaida.
mdau akinyunyizia dawa ya ukungu kwenye mitikiti

CHANGAMOTO!!

Mimea iliendelea vizuri sana mpaka nikawa najipa moyo kuwa kulimo hiki nimekipatia kwelikweli mpaka pale changamoto halisi zilipoanza kujitokeza,na hapo ndipo nilipogundua wengi hukata tamaa na kilimo.Ilikuwa ni wiki moja tangu mimea yetu ichipue na ilikuwa ni yenye afya nzuri kabisa.Nikiwa nazungukia shamba nikagundua mimea mingi sana ikiwa imekatwa na kubaki shina na jani la juu halionekani.Lakini pia niligundua kuwa kila sehemu iliyoathilika pembeni yake kulikuwa na vijishimo vidogo vidogo.
Moja ya vijishimo karibu na mimea iliyoathiriwa


Baada ya kugundua tatizo  tulilonalo wenyeji wangu walibaini kuwa mdudu anaetusumbua ni mdudu aitwae KIYENZE....mdudu huyu hakuweza kuuawa na madawa tuliyokuwa tukitumia kwenye mimea yetu hivyo ilitubidi tufanye njia mbadala ili tuweze kudhibiti tatizo.Ilitubidi tuchimbe kila sehemu tulipoona kuna vijishimo vidogo na sehemu kubwa tulifanikiwa kuwatoa hao VIYENZE na pia tulikuta mimea mingi imekatwa na kuhifadhiwa kwenye mashimo na hao viyenze.

Baada ya tatizo hilo kujitokeza tuligundua umuhimu wa kupanda mbegu mbilimbili mpaka tatu kwenye eneo moja kwa vile sehemu ilipokatwa mche mmoja basi mche mwingine ulibaki na shughuli yetu iliendelea kama kawaida.Lakini pia nilijifunza kuwa mdudu huyu unaweza kumdhibiti katika hatua za awali kabisa kabla hajaanza kuleta madhara kwenye mimea yako kwa vile uwepo wake unapambanuliwa na vijishimo vidogo vidogo kama nilivyoonesha kwenye picha hapo juu..

Sunday 24 January 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA. Na yohana maduhu

SEHEMU YA PILI

Hatua ya kwanza

baada ya siku nne mpaka tano mbegu zetu zilianza kumea,hivyo kazi kubwa iliyokuwepo ni umwagiliaji.tulimwagilia mala mbili kwa siku japo sio vibaya ukimwagilia maji mengi mara moja kwa siku

KAZI TU!!....
Hatua hii ya umwagiliaji iliibua changamoto kadhaa wa kadhaa ikiwamo ya kazi ngumu yenyewe ya umwagiliaji hasa kutokana na ukubwa wa shamba na vitendea kazi duni.Tulikuwa tukivuta maji kwa waterpump kutoka kwenye mto uliokuwa umbali wa mita 100 mpaka shambani kwetu tulipokuwa tumeandaa bwawa kwa ajiri ya kuhifadhia maji.Kutoka kwenye bwawa letu tulichota maji kwa kutumia ndoo kwa ajiri ya umwagiliaji.
                                       
                          Picha ya juu na chini zinaonesha tukiandaa mashine
                                kwa ajili ya kuvuta maji kutoka kwenye mto
                                     kuelekea kwenye bwawa la shambani
                            Maji kutokea mtoni yakiingia kwenye bwawa letu
                           Kijana akichota maji tayari kwa umwagiliaji wa mazao

                                      Vijana wakiwa bize kumwagilia tikitimaji...