Thursday 4 February 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA

SEHEMU YA TATU

Palizi ya kwanza na uwekaji wa mbolea

Katika sehemu hii ya kilimo chetu shughuli kubwa ilikuwa utunzaji wa shamba letu ambapo kazi kubwa ilikuwa kumwagilia mimea,kupulizia dawa.Kikubwa zaidi shughuli ya palizi ya kwanza ilianza rasmi,kwa vile mimea ilikuwa na wiki tatu hivyo majani yasiyohitajika yalikuwa yameanza kumea karibu na mimea yetu.Kazi ya palizi iliendana na uwekaji wa mbolea .
Tulitumia mbolea aina ya NPK kwa ajiri ya kukuzia mimea,japo katika hatua hii nilitembelea wakulima wengine na kukuta kila mmoja ana formula yake ya aina gani ya mbolea itumike katika hatua hiyo.Baadhi walitumia samadi iliyooza vizuri na wengine walitumia KANI,.sisi tulitumia NPK.

                                Mdau akipalilia palizi ya kwanza katika shamba la tikiti maji

                                           Mdau akiweka mbolea aina ya NPK baada palizi

  Baada ya uwekaji wa mbolea tuliendelea na umwagiliaji wa mimea yetu na baada ya wiki moja tena mimea yetu ilikuwa imekuwa kwa kiasi kikubwa na kuanza kutambaa.
                                        Mdau akipulizia dawa ya kuua wadudu katika mimea.


Ningependa kuwaeleza wasomaji mbalimbali wa makala hii kuwa,ukizingatia matumizi ya dawa za ukungu na wadudu katika kilimo cha matikiti maji utakumbana na changamoto chache sana.japo kuna changamoto zingine ni za mazingila husika kama vile hali ya hewa.mfano kuna maeneo mimea inaathiliwa sana na ukungu au utitili,hivyo matumizi ya dawa yanapaswa yawe ni ya mala kwa mala.
Picha zifuatazo hapo chini ni kati ya madhara ya wadudu katika matikiti maji...

                                            mmea ulioshambuliwa na wadudu waharibifu



                              Mmea ulioshambuliwa na utitiri mweusi ambao hukaa chini ya tawi

Kwa kawaida mimea iliyoathilika kwa kiwango hicho hapo juu inanafasi ya kuambukiza mimea mingine,Hivyo ni bora mkulima akiwa anapulizia dawa mala kwa mala ili kuepuka athali hizo,lakini pia mimea hiyo inaweza kupona kama ikipata huduma ya madawa




No comments:

Post a Comment