Tuesday 9 February 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA

SEHEMU YA NNE

palizi ya pili na uwekaji wa mbolea

Baada ya mwezi mmoja na wiki mbili mimea na nyasi zisizohitajika vilikuwa vimeshaota hivyo ulikuwa ni wakati muafaka wa kufanya palizi kwa mara ya pili.Tulipalilia lakini pia tuliweka mbolea kwenye mimea yetu na safari hii sikuweka mbolea za madukani bali nilitumia mbolea ya samadi iliyooza vizuri.
                                          Nikishiriki kikamilifu zoezi la uwekaji wa mbolea


Wadau wakiweka samadi katika mitikiti maji.

Katika hatua zote hizi shughuli ya umwagiliaji ilikuwa ni ya kila siku,pia zoezi la upuliziaji wa madawa lilikuwa likiendelea na tulikuwa tukipulizia dawa mara moja kwa wiki.

MBOLEA YA MAJANI

Katika kipindi hiki pia tulitembelewa na bwana shamba ambae alitupatia ushauri wa kuanza kutumia mbolea ya kunyunyizia kwenye majani ya mimea yetu,mbolea hizi lengo lake ni kurutubisha jani la mmea na tunda,na katika hatua hii matunda yalikuwa yameshaanza kutokeza kwa wingi.kwa kawaida zipo aina nyingi za mbolea za namna hiyo japo sisi tulitumia NPK,hii inapatikana katika mfumo wa unga unga hivyo unapaswa kuichanganya na maji kwa kutumia maelekezo stahiki na kunyunyiza kwenye majani.

Matunda machanga katika mimea
Mdau akinyunyiza mbolea ya majani katika mimea

Tuliendelea kufuatilia mimea yetu kwa karibu sana na tulipogundua tatizo lolote tuliwahi kulitatua kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.Nilijifunza mambo mbalimbali kupitia kwenye mitandao pamoja na kufuata ushauri wa wataalamu(mabwana na bibi shamba) na baada ya miezi miwili shamba letu lilikuwa linapendeza na lilibeba matunda ya kutosha na yenye afya nzuri kabisa











No comments:

Post a Comment