Monday 15 February 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA

Sehemu ya tano(mwisho)

UVUNAJI WA MATUNDA

Baada ya siku sabini tulisitisha umwagiliaji katika shamba letu kwa muda wa wiki moja kabla ya uvunaji,hii inasaidia kufanya matunda yajitengenezee sukari na kuyafanya kuwa matamu zaidi,pia inasaidia kuepusha kupasuka kwa matunda.Huu ni ushauri ambao tulipewa na Bwana shamba.
Baada ya siku sabini na tano(unaweza kuenda mpaka siku themanini)shamba letu lilikuwa tayari kwa ajiri ya kuvuna na tulianza shughuli ya uvunaji.
Kilichonishangaza na kunifurahisha ni kwamba siku ya uvunaji nilipata kampani kubwa sana kuliko kipindi chote,karibu kijiji kizima kilikuja kunisaida kuvuna,watoto kwa wazee.

                                          vijana wakivuna matikiti maji shambani



picha za juu,vijana wakipakia matikiti maji kwenye gari tayari kwa kupeleka sokoni


SOKO
Wakati wa kuvuna mazao yetu walikuja wafanyabiashara mbalimbali kutaka kununua mazao yote.Hawa jamaa kwa kawaida humpunja mkulima ili wao wapate faida kubwa zaidi(mpaka mara tatu au nne ya bei waliyonunulia).Hivyo sisi tulikuwa tumejipanga kuuza wenyewe sokoni.Tulikodisha canter mbili tukasomba mzigo wote na kuupeleka katika soko la Buhongwa ambalo ni karibu zaidi.Tuliomba nafasi kwenye uongozi wa soko na kuweka bidhaa zetu na kuanza kuuza kwa jumla na rejareja na mimi mwenyewe nikiwa msimamizi mkuu.Kwavile kulikuwa na uhaba wa matikiti maji sokoni kwa kipindi hicho tuliweza kumaliza mzigo wetu ndani ya wiki moja tu na mauzo yetu yalikuwa ni jumla ya shilingi millioni nane.Gharama zote nilizotumia hazikufika millioni moja.Hivyo basi nilitengeneza shillingi millioni saba kwa muda wa miezi mitatu tena kwa kilimo nilichokifanya kwa mara ya kwanza na pasipo uzoefu wowote.
KAMA UNATAKA MALI UTAYAPATA SHAMBANI.

Tuesday 9 February 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA

SEHEMU YA NNE

palizi ya pili na uwekaji wa mbolea

Baada ya mwezi mmoja na wiki mbili mimea na nyasi zisizohitajika vilikuwa vimeshaota hivyo ulikuwa ni wakati muafaka wa kufanya palizi kwa mara ya pili.Tulipalilia lakini pia tuliweka mbolea kwenye mimea yetu na safari hii sikuweka mbolea za madukani bali nilitumia mbolea ya samadi iliyooza vizuri.
                                          Nikishiriki kikamilifu zoezi la uwekaji wa mbolea


Wadau wakiweka samadi katika mitikiti maji.

Katika hatua zote hizi shughuli ya umwagiliaji ilikuwa ni ya kila siku,pia zoezi la upuliziaji wa madawa lilikuwa likiendelea na tulikuwa tukipulizia dawa mara moja kwa wiki.

MBOLEA YA MAJANI

Katika kipindi hiki pia tulitembelewa na bwana shamba ambae alitupatia ushauri wa kuanza kutumia mbolea ya kunyunyizia kwenye majani ya mimea yetu,mbolea hizi lengo lake ni kurutubisha jani la mmea na tunda,na katika hatua hii matunda yalikuwa yameshaanza kutokeza kwa wingi.kwa kawaida zipo aina nyingi za mbolea za namna hiyo japo sisi tulitumia NPK,hii inapatikana katika mfumo wa unga unga hivyo unapaswa kuichanganya na maji kwa kutumia maelekezo stahiki na kunyunyiza kwenye majani.

Matunda machanga katika mimea
Mdau akinyunyiza mbolea ya majani katika mimea

Tuliendelea kufuatilia mimea yetu kwa karibu sana na tulipogundua tatizo lolote tuliwahi kulitatua kwa kufuata ushauri wa kitaalamu.Nilijifunza mambo mbalimbali kupitia kwenye mitandao pamoja na kufuata ushauri wa wataalamu(mabwana na bibi shamba) na baada ya miezi miwili shamba letu lilikuwa linapendeza na lilibeba matunda ya kutosha na yenye afya nzuri kabisa











Thursday 4 February 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA

SEHEMU YA TATU

Palizi ya kwanza na uwekaji wa mbolea

Katika sehemu hii ya kilimo chetu shughuli kubwa ilikuwa utunzaji wa shamba letu ambapo kazi kubwa ilikuwa kumwagilia mimea,kupulizia dawa.Kikubwa zaidi shughuli ya palizi ya kwanza ilianza rasmi,kwa vile mimea ilikuwa na wiki tatu hivyo majani yasiyohitajika yalikuwa yameanza kumea karibu na mimea yetu.Kazi ya palizi iliendana na uwekaji wa mbolea .
Tulitumia mbolea aina ya NPK kwa ajiri ya kukuzia mimea,japo katika hatua hii nilitembelea wakulima wengine na kukuta kila mmoja ana formula yake ya aina gani ya mbolea itumike katika hatua hiyo.Baadhi walitumia samadi iliyooza vizuri na wengine walitumia KANI,.sisi tulitumia NPK.

                                Mdau akipalilia palizi ya kwanza katika shamba la tikiti maji

                                           Mdau akiweka mbolea aina ya NPK baada palizi

  Baada ya uwekaji wa mbolea tuliendelea na umwagiliaji wa mimea yetu na baada ya wiki moja tena mimea yetu ilikuwa imekuwa kwa kiasi kikubwa na kuanza kutambaa.
                                        Mdau akipulizia dawa ya kuua wadudu katika mimea.


Ningependa kuwaeleza wasomaji mbalimbali wa makala hii kuwa,ukizingatia matumizi ya dawa za ukungu na wadudu katika kilimo cha matikiti maji utakumbana na changamoto chache sana.japo kuna changamoto zingine ni za mazingila husika kama vile hali ya hewa.mfano kuna maeneo mimea inaathiliwa sana na ukungu au utitili,hivyo matumizi ya dawa yanapaswa yawe ni ya mala kwa mala.
Picha zifuatazo hapo chini ni kati ya madhara ya wadudu katika matikiti maji...

                                            mmea ulioshambuliwa na wadudu waharibifu



                              Mmea ulioshambuliwa na utitiri mweusi ambao hukaa chini ya tawi

Kwa kawaida mimea iliyoathilika kwa kiwango hicho hapo juu inanafasi ya kuambukiza mimea mingine,Hivyo ni bora mkulima akiwa anapulizia dawa mala kwa mala ili kuepuka athali hizo,lakini pia mimea hiyo inaweza kupona kama ikipata huduma ya madawa




Tuesday 26 January 2016

SEHEMU YA PILI

Hatua ya pili

Katika hatua hii tulianza rasmi kulinda mimea yetu dhidi ya wadudu na magonjwa mbalimbali,na mbaka muda huo tulikua tunajua adui zetu wakubwa ni ukungu pamoja na utitiri(mwekundu au mweusi),hivyo tulinunua madawa ya ukungu pamoja na madawa ya kuua wadudu wanaoweza kushambulia mimea yetu.Tulikuwa tukipulizia dawa ya ukungu mara moja kwa wiki na hata dawa ya wadudu(sumu)tulipulizia mara moja kwa wiki.Lakini hizi dawa hazikutumika kwa wakati mmoja,sumu ya wadudu ilitumika peke yake kwa wakati wake(siku tofauti)na dawa ya ukungu ilitumika tofauti kwa wakati wake.Wakati huo huo kazi ya umwagiliaji iliendelea kama kawaida.
mdau akinyunyizia dawa ya ukungu kwenye mitikiti

CHANGAMOTO!!

Mimea iliendelea vizuri sana mpaka nikawa najipa moyo kuwa kulimo hiki nimekipatia kwelikweli mpaka pale changamoto halisi zilipoanza kujitokeza,na hapo ndipo nilipogundua wengi hukata tamaa na kilimo.Ilikuwa ni wiki moja tangu mimea yetu ichipue na ilikuwa ni yenye afya nzuri kabisa.Nikiwa nazungukia shamba nikagundua mimea mingi sana ikiwa imekatwa na kubaki shina na jani la juu halionekani.Lakini pia niligundua kuwa kila sehemu iliyoathilika pembeni yake kulikuwa na vijishimo vidogo vidogo.
Moja ya vijishimo karibu na mimea iliyoathiriwa


Baada ya kugundua tatizo  tulilonalo wenyeji wangu walibaini kuwa mdudu anaetusumbua ni mdudu aitwae KIYENZE....mdudu huyu hakuweza kuuawa na madawa tuliyokuwa tukitumia kwenye mimea yetu hivyo ilitubidi tufanye njia mbadala ili tuweze kudhibiti tatizo.Ilitubidi tuchimbe kila sehemu tulipoona kuna vijishimo vidogo na sehemu kubwa tulifanikiwa kuwatoa hao VIYENZE na pia tulikuta mimea mingi imekatwa na kuhifadhiwa kwenye mashimo na hao viyenze.

Baada ya tatizo hilo kujitokeza tuligundua umuhimu wa kupanda mbegu mbilimbili mpaka tatu kwenye eneo moja kwa vile sehemu ilipokatwa mche mmoja basi mche mwingine ulibaki na shughuli yetu iliendelea kama kawaida.Lakini pia nilijifunza kuwa mdudu huyu unaweza kumdhibiti katika hatua za awali kabisa kabla hajaanza kuleta madhara kwenye mimea yako kwa vile uwepo wake unapambanuliwa na vijishimo vidogo vidogo kama nilivyoonesha kwenye picha hapo juu..

Sunday 24 January 2016

NILIPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA. Na yohana maduhu

SEHEMU YA PILI

Hatua ya kwanza

baada ya siku nne mpaka tano mbegu zetu zilianza kumea,hivyo kazi kubwa iliyokuwepo ni umwagiliaji.tulimwagilia mala mbili kwa siku japo sio vibaya ukimwagilia maji mengi mara moja kwa siku

KAZI TU!!....
Hatua hii ya umwagiliaji iliibua changamoto kadhaa wa kadhaa ikiwamo ya kazi ngumu yenyewe ya umwagiliaji hasa kutokana na ukubwa wa shamba na vitendea kazi duni.Tulikuwa tukivuta maji kwa waterpump kutoka kwenye mto uliokuwa umbali wa mita 100 mpaka shambani kwetu tulipokuwa tumeandaa bwawa kwa ajiri ya kuhifadhia maji.Kutoka kwenye bwawa letu tulichota maji kwa kutumia ndoo kwa ajiri ya umwagiliaji.
                                       
                          Picha ya juu na chini zinaonesha tukiandaa mashine
                                kwa ajili ya kuvuta maji kutoka kwenye mto
                                     kuelekea kwenye bwawa la shambani
                            Maji kutokea mtoni yakiingia kwenye bwawa letu
                           Kijana akichota maji tayari kwa umwagiliaji wa mazao

                                      Vijana wakiwa bize kumwagilia tikitimaji...                                                                                                                

Saturday 6 June 2015

NILIAPOFANYA KILIMO CHA MATIKITI MAJI KWA MARA YA KWANZA. Na yohana maduhu

Sehemu ya kwanza:
Kwa jina naitwa yohana maduhu,nimkazi wa mwanza..katika maisha yangu nimekuwa na imani kubwa na shughuli za kilimo na ufugaji kama ndio chanzo chepesi zaidi cha kujipatia kipato halali,japo mtu anaweza kuamini tofauti na ninavyo amini mimi…tatizo kubwa lililopo kwa wakulima wengi ni kutokujua thamani ya kazi yao hivyo wafanyabiashara wengi wamekuwa wakinunua bidhaa zao kwa bei ya chini sana harafu wao wanauza kwa bei ya juu.Mfano chungwa moja la wastani linaweza kuuzwa sokoni kwa shilingi mia mbili,wakati mlanguzi kanunua kwa mkulima machungwa kumi ya aina hiyo kwa shilingi mia mbili,huo ni mfano mdogo tu,japo muuzaji wa sokoni analipa ushuru lakini ushuru huo ni mdogo tu ambao hata mkulima anaweza kustahimili kuulipa.
Nilikuwa sijawahi kufanya kilimo chochote katika maisha yangu,ila nikadhamilia kuingia katika kilimo kwa lengo la kupata faida ya juu kabisa(maximum profit)ya kile ntakachozalisha.na wazo langu likanipeleka kufanya kilimo cha matikiti maji.na sababu ya kuchagua matikiti maji ni kama ifuatavyo: kwanza kabisa yanakomaa kwa muda mfupi,(miezi miwili hadi mitatu)hivyo sitasubili saana kupata faida yangu,pili ni matunda ambayo watu wengi wanayapenda,mimi nikiwa mmoja wao. Lakini pia nilitamani sana nisikosee,hivyo nilidhamilia kuhusisha wataaramu katika kila hatua ikiwa ni pamoja na kusoma kwenye mitandao habari mbalimbali zinazohusu kilimo cha matikiti maji. Nilifuata hatua zifuatazo:
HATUA YA KWANZA.
kutafuta shamba.
Hii ilikuwa ni hatua ya kutafuta shamba ,nilikwenda sehemu moja inaitwa usagala,nje kidogo ya jiji la mwanza na kukodi shamba la heka tatu kwa kiasi cha shilingi laki moja (kubargain muhimu) .kwa kuzingatia ukaribu na uwepo wa vyanzo vya maji.pia nilizingatia aina ya udongo kwa vile nilishajua matikiti maji yanastawi vizuri zaidi katika ardhi ya kichanga na sababu kubwa ikiwa ni kutotuamisha maji kwa ardhi ya kichanga.kwani maji yakiwa yanatuama husababisha matunda kuoza.

            Nikiwa shambani kuhakikisha kama linafaa kwa kilimo cha matikiti

Nikiwa tayari kwa ajiri ya maandalizi ya kilimo

HATUA YA PILI
Hii ilikuwa ni hatua ya kuandaa shamba,niliajiri wanakijiji wakalima eneo lote la heka tatu kwa kutumia maksai,pamoja na majembe ya mkono kwa ajili ya kupanga matuta.hatua hii ilinighalimu kiasi cha shilingi laki moja na nusu.hapa maksai wanatifua aldhi harafu majembe ya mkono yanatengeneza matuta(kama kawa nililia shida nikapunguziwa).

Ili  kazi iende vizuri nilifanya mpango tukawa tunapika chakula na kila mtu alikuwa anafurahi.hii inasaidia kupunguza movements wakati wa kazi,na pia inawatia moyo wafanyakazi na zaidi ikanijengea uhusiano mzuri na wao.wakati mwingine tatizo linaweza kutokea,wanakuwa upande wako.

HATUA YA TATU
upandaji
Katika ununuzi wa mbegu kwa mara ya kwanza ndo nilikutana na neno highbreed(mbegu chotara,zilizo tengenezwa kitaaram kutoa mazao mengi na bora)sikuweza kununua mbegu hizo kwa vile zilikuwa na gharama kubwa na mimi kwa vile ndo kilimo cha kwanza sikutaka kuingia gharama kubwa kwa kitu ambacho sijui matokeo yake(japo sikushauri ufanye kama mimi).niliamua kununua mbegu ya kawaida aina ya sugar baby,inayokomaa kwa siku sabini hadi themanini.pia matunda yake yanaukubwa wa wastani,hapa niligharamika kiasi cha shilingi elfu hamsini kwa ajiri ya manunuzi ya mbegu.katika upandaji tulikuwa tunaweka mbolea ya samadi iliyooza vizuri kwenye kila shimo na kuichanganya vizuri na udongo,tulihakikisha tuna panda mbegu mbili mbili kila shimo umbali wa sentimita mbili chini ya udongo kwa umbali wa sentimita 30 toka shina hadi shina na mita 1.5-2 kutoka mstari hadi mstari, kwavile wanakijiji washakuwa rafiki zangu walinipandia mbegu bila gharama yeyote,kuwaonesha ninajari nikaungurumisha ugali wa maana na dagaa za kutosha tukala tukashiba,na burudani za hapa na pale hazikukosa.




INAENDELEA....

Tuesday 2 June 2015

KUTANA NA MFUGAJI ALIYEANZA KWA KUSOMA KITABU CHA UJASILIAMALI HADI KUWA MFUGAJI MKUBWA

"Baada ya kuona maisha yanakuwa magumu,niliumiza kichwa  nifanye shughuli gani ili niongeze kipato changu,hivyo nikaamua kununua kitabu cha ujasiliamali na kujifunza kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji"....haya ni maneno ya bwana Alfonce Emmanuel ambae ni mkazi wa jijini Mwanza maeneo ya kiseke.

Bwana alfonce akilisha kuku zake

 Akiendelea kutufahamisha jinsi alivyoanza shughuli za ufugaji Bwana alfonce anasema alianza na kuku wanane tu,saba wakiwa majike na jogoo mmoja ambao aliwanunua kwa umakini wa kuzingatia mbegu bora kutoka kwa jirani yake ambae nae alikuwa mfugaji
lakini nini cha tofauti kwa alphonce ni jinsi ya yeye anavyo wapata kuku wake." mimi na totolesha kuku mwenyewe kwa kuwapa matetea mayai na wiki moja baada ya vifaranga kutotolewa navitoa kwa matetea na kuwa weka katika chumba ambacho watapata joto lakutosha na kukua wakati huo nawapa pumba laini ama chenga ndogondogo sana za mchele na katika maji yao nawachanganyia vitamini na groucouse  "alisema  alphonce.

Chumba cha kuhifadhia vifaranga wa wiki moja hadi mwezi mmoja

"baada ya mwezi mmoja navichukua vifaranga na kuviweka katika mabanda katika chumba kingine, chumba hiki kimegawanyika katika mabanda mawili ikiwa ni moja kwajili ya kuku wa mwezi mmoja na lingine mwenzi wa pili wakati kuku walioko chini ya mabanda haya ni kuku walio zidi miezi mitatu amabao wako tayari kuchanganywa na kuku wengine wakubwa. nafanya hivi kwa sababu ya kuwaepusha kuku na magonjwa, maana kama vifaranga vya mwenzi mmoja havina kinga ya mwili ya kutosha hivyo ukiviweka na kuku wakubwa ni rahisi kupata magonjwa na kufa". alphoince.

Chumba cha vifaranga wa mwezi mmoja hadi miwili.

"huwa natumia chakula cha kawaida kwa maana ya pumba za mahindi, mchicha na dagaa pamoja na vyakula vingine vya kuku kama konokono na mashudu.
lakini changamoto kubwa ni magonjwa ya kuku,kila baada ya miezi mitatu huwa nawapa chanjo ya kideli ambayo ni Newcastle. pia kwa vifaranga huwa nawapa chanjo ya ndui mara tu wafikishapo wiki mbili.pamoja na hayo najitahidi kuwatibu pale wanapopata magonjwa kama mafua kwa kuwapa dawa za mafua kama vile fluban.kwa kifupi nakuwa karibu zana na mifugo yangu hiyo ili kujua tatizo..vilevile ninapogundua kunakuku anaugonjwa huwa namtenganisha na wengine ili asiwaambukize.
kutokana na uzoefu nilionao kwa sasa ninauwezo wa kupambanua magonjwa ya kuku kwa kuangalia aina ya kinyesi cha kuku na hata muonekano wa kuku.mfano kinyesi kikiwa cha kijani basi kuku anatatizo la mafua,japo kwa tatizo hilohilo kuku anaweza kua anapiga chafya.na ni bora mfugaji yeyote kuyajua magonjwa ya kuku na dawa zake.".



kwa kiasi kikuibwa faida yake inatokana na kuuza kuku na mara nyingine kuuza mayai japo bwana alfonce yeye anadai hauzi mayai,ila anachofanya ni kuyatotoresha ili awe na kuku wengi. kuku moja mkubwa anauza 10000 kwa mtetea na 15000 kwa jogoo japo bei huongezeka kipindi cha sikukuu.zaidi huwauza  kuku hao kwa jumla kwa wafugaji wengine.